17 “Na lazima Edomu awe kitu cha kutisha.+ Kila mtu anayepita kando yake atatazama kwa hofu na kupiga mluzi kwa sababu ya mapigo yake yote. 18 Kama Sodoma na Gomora na miji jirani ilivyoangamizwa,”+ Yehova anasema, “hakuna mtu atakayekaa huko, na hakuna mtu atakayeishi huko.+
13 kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Pia nitaunyoosha mkono wangu dhidi ya Edomu na kuwaangamiza wanadamu na wanyama waliomo, nami nitaifanya kuwa ukiwa.+ Kuanzia Temani mpaka Dedani, watauawa kwa upanga.+
4 “Ingawa Waedomu wanasema, ‘Tumevunjwavunjwa, lakini tutarudi na kujenga tena magofu,’ Yehova wa majeshi anasema hivi: ‘Watajenga, lakini nitabomoa, nao wataitwa “eneo la uovu” na “watu ambao Yehova amewahukumu milele.”+