Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ezekieli 25:12, 13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Nchi ya Edomu imelipiza kisasi dhidi ya nyumba ya Yuda nayo imepata hatia kubwa kwa kulipiza kisasi dhidi yake;+ 13 kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Pia nitaunyoosha mkono wangu dhidi ya Edomu na kuwaangamiza wanadamu na wanyama waliomo, nami nitaifanya kuwa ukiwa.+ Kuanzia Temani mpaka Dedani, watauawa kwa upanga.+

  • Ezekieli 35:10, 11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 “Kwa sababu ulisema, ‘Mataifa haya mawili na nchi hizi mbili zitakuwa zangu, nasi tutazimiliki zote mbili,’+ hata ingawa Yehova mwenyewe alikuwa humo, 11 ‘kwa hiyo kwa hakika kama ninavyoishi,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘nitakutendea kulingana na hasira ileile na wivu uleule ulioonyesha ulipowachukia;+ nami nitajijulisha miongoni mwao nitakapokuhukumu.

  • Amosi 1:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Yehova anasema hivi:

      ‘Kwa sababu ya maasi matatu ya Edomu,+ na hata manne, sitabadili uamuzi wangu,

      Kwa sababu alimfuatia kwa upanga ndugu yake mwenyewe,+

      Na kwa sababu alikataa kuonyesha rehema;

      Katika hasira yake anaendelea kuwararuararua bila huruma,

      Na bado anaendelea kuwakasirikia vikali.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki