Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 40:29
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 29 Akaweka madhabahu ya dhabihu za kuteketezwa+ kwenye mlango wa hema la ibada, yaani, hema la mkutano, ili atoe juu yake dhabihu za kuteketezwa+ na matoleo ya nafaka, kama Yehova alivyomwamuru Musa.

  • Mambo ya Walawi 1:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 “‘Kisha huyo ng’ombe dume mchanga atachinjwa mbele za Yehova, nao wana wa Haruni, makuhani,+ wataleta damu ya mnyama huyo na kuinyunyiza pande zote za madhabahu,+ kwenye mlango wa hema la mkutano.

  • Mambo ya Walawi 8:18-21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Halafu akamleta kondoo dume wa dhabihu ya kuteketezwa, Haruni na wanawe wakaweka mikono yao juu ya kichwa cha kondoo dume huyo.+ 19 Musa akamchinja na kunyunyiza damu yake pande zote za madhabahu. 20 Akamkata kondoo huyo vipandevipande, akateketeza kichwa, vipande alivyokata, na mafuta yaliyo kwenye figo, ili vifuke moshi. 21 Akaosha matumbo na miguu kwa maji na kumteketeza kondoo dume mzima kwenye madhabahu ili afuke moshi. Ilikuwa dhabihu ya kuteketezwa yenye harufu inayopendeza.* Ilikuwa dhabihu kwa Yehova inayochomwa kwa moto, kama Yehova alivyomwamuru Musa.

  • Ezekieli 45:19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 Kuhani atachukua sehemu ya damu ya dhabihu ya dhambi na kuiweka kwenye mwimo wa mlango wa hekalu,+ juu ya zile pembe nne za ukingo unaozunguka madhabahu, na juu ya mwimo wa lango la ua wa ndani.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki