-
2 Wafalme 23:8, 9Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
8 Kisha akawaondoa makuhani wote katika majiji ya Yuda, naye akafanya mahali pa juu ambapo makuhani walifukizia moshi wa dhabihu pasifae kwa ibada, kuanzia Geba+ mpaka Beer-sheba.+ Alibomoa pia mahali pa juu palipokuwa kwenye malango yaliyokuwa katika njia ya kuingia kwenye lango la Yoshua mkuu wa jiji, malango yaliyokuwa upande wa kushoto mtu anapoingia katika lango la jiji. 9 Makuhani wa mahali pa juu hawakuhudumu kwenye madhabahu ya Yehova kule Yerusalemu,+ lakini walikula mikate isiyo na chachu pamoja na ndugu zao.
-