-
Hesabu 28:9, 10Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
9 “‘Hata hivyo, siku ya Sabato,+ mnapaswa kutoa wanakondoo dume wawili wasio na kasoro wenye umri wa mwaka mmoja pamoja na toleo la nafaka la sehemu mbili za kumi za kipimo cha efa ya unga laini uliochanganywa na mafuta, pamoja na toleo lake la kinywaji. 10 Hiyo ndiyo dhabihu ya kuteketezwa ya Sabato, pamoja na dhabihu ya kuteketezwa inayotolewa kwa ukawaida pamoja na toleo lake la kinywaji.+
-
-
Ezekieli 45:17Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
17 Lakini kiongozi atakuwa na wajibu wa kushughulikia dhabihu nzima za kuteketezwa,+ toleo la nafaka,+ na toleo la kinywaji wakati wa sherehe,+ miezi mipya, Sabato,+ na sherehe zote zilizoamriwa za nyumba ya Israeli.+ Yeye ndiye atakayetoa dhabihu ya dhambi, toleo la nafaka, dhabihu nzima ya kuteketezwa, na dhabihu za ushirika, ili kufunika dhambi za watu wa nyumba ya Israeli.’
-