16 Manase pia alimwaga damu nyingi sana isiyo na hatia mpaka alipojaza Yerusalemu damu hiyo kutoka mwisho mmoja hadi mwingine,+ mbali na dhambi yake aliyosababisha Yuda kutenda kwa kufanya maovu machoni pa Yehova.
3 Hakika watu wa Yuda walipatwa na mambo hayo kwa agizo la Yehova, ili kuwaondoa mbele za macho yake+ kwa sababu ya dhambi zote ambazo Manase alitenda,+4 na pia kwa sababu ya damu isiyo na hatia aliyomwaga,+ kwa maana alijaza Yerusalemu damu isiyo na hatia na Yehova hakutaka kumsamehe.+
9 Basi akaniambia: “Kosa la watu wa nyumba ya Israeli na Yuda ni kubwa sana, kubwa kwelikweli.+ Nchi imejaa umwagaji wa damu,+ nalo jiji limejaa ufisadi.+ Kwa maana wanasema, ‘Yehova ameiacha nchi hii, na Yehova haoni.’+