-
Kutoka 34:6, 7Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
6 Yehova alipita mbele yake akitangaza: “Mimi Yehova, Yehova, ni Mungu mwenye rehema+ na huruma,*+ si mwepesi wa hasira,+ nina upendo mwingi mshikamanifu*+ na kweli,*+ 7 ninawatendea maelfu kwa upendo mshikamanifu,+ ninasamehe makosa na uovu na dhambi,+ lakini sikosi kamwe kuwaadhibu wenye hatia,+ ninawaadhibu wana na wajukuu kufikia kizazi cha tatu na cha nne kwa sababu ya makosa ya baba zao.”+
-
-
Nehemia 9:17Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
17 Walikataa kusikiliza+ wala hawakukumbuka matendo yako ya ajabu uliyofanya miongoni mwao, lakini wakawa wakaidi,* nao wakachagua kiongozi ili warudi Misri ambako walikuwa watumwa.+ Lakini wewe ni Mungu uliye tayari kusamehe,* mwenye huruma* na rehema, usiye mwepesi wa hasira, una upendo mwingi mshikamanifu,*+ nawe hukuwaacha.+
-