-
Danieli 4:23-26Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
23 “‘Wewe mfalme ulimwona mlinzi, mtakatifu,+ akishuka kutoka mbinguni, aliyekuwa akisema: “Ukateni na kuuangusha chini mti huu na kuuharibu, lakini kiacheni kisiki na mizizi yake ardhini kikiwa na pingu ya chuma na ya shaba, katikati ya majani ya shambani. Na acheni umande wa mbinguni ukiloweshe, na acheni fungu lake liwe pamoja na wanyama wa mwituni mpaka nyakati saba zipite.”+ 24 Ee mfalme, hii ndiyo maana yake; ni agizo la Aliye Juu Zaidi ambalo lazima litimie kwako bwana wangu mfalme. 25 Utafukuzwa mbali kutoka miongoni mwa wanadamu, utaishi na wanyama wa mwituni, nawe utapewa majani ule kama ng’ombe dume; na utalowa kwa umande wa mbinguni,+ na nyakati saba+ zitapita,+ mpaka utakapojua kwamba Aliye Juu Zaidi ni Mtawala katika ufalme wa wanadamu na kwamba yeye humpa ufalme huo yeyote anayetaka kumpa.+
26 “‘Lakini kwa sababu walisema kisiki cha mti huo kiachwe pamoja na mizizi yake,+ utarudishiwa tena ufalme wako baada ya kujua kwamba mbingu zinatawala.
-