Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Samweli 2:7, 8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  7 Yehova humfanya mtu awe maskini, naye hutajirisha;+

      Hushusha, naye hukweza.+

       8 Humwinua mtu wa hali ya chini kutoka mavumbini;

      Humwinua maskini kutoka katika rundo la majivu,*+

      Ili awafanye wakae pamoja na wakuu,

      Na kuwapa kiti cha heshima.

      Nguzo za dunia ni za Yehova,+

      Naye huweka nchi inayozaa juu yake.

  • Ayubu 34:24
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 Huwapondaponda wenye nguvu bila kuhitaji kufanya uchunguzi

      Na kuwaweka wengine mahali pao.+

  • Yeremia 27:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 ‘Mimi ndiye niliyeiumba dunia, wanadamu, na wanyama walio duniani kwa nguvu zangu kuu na kwa mkono wangu ulionyooshwa; nami nimempa yeyote ninayetaka.*+

  • Ezekieli 21:26, 27
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Kiondoe kilemba, na ulivue taji.+ Hili halitabaki kama lilivyo.+ Mwinue aliye chini,+ na umshushe aliye juu.+ 27 Nitaliharibu, nitaliharibu, nitaliharibu. Nalo halitakuwa la mtu yeyote mpaka yule aliye na haki ya kisheria atakapokuja,+ nami nitampa yeye.’+

  • Danieli 2:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 Yeye hubadili nyakati na majira,+

      Huwaondoa wafalme na kuwaweka wafalme,+

      Huwapa hekima walio na hekima na kuwapa ujuzi wale walio na utambuzi.+

  • Danieli 7:13, 14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 “Nikaendelea kuangalia katika maono ya usiku, na tazama! mtu fulani kama mwana wa binadamu+ alikuwa akija na mawingu ya mbinguni; naye akaja mbele za Mzee wa Siku,+ nao wakamleta karibu Naye. 14 Naye akapewa utawala,+ heshima,+ na ufalme, ili watu wa makabila, mataifa, na lugha zote wamtumikie.+ Utawala wake ni utawala wa milele ambao hautapitilia mbali, na ufalme wake hautaangamizwa.+

  • Luka 1:32, 33
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 32 Huyo atakuwa mkuu+ naye ataitwa Mwana wa Aliye Juu Zaidi,+ na Yehova* Mungu atampa kiti cha ufalme cha Daudi baba yake,+ 33 naye atatawala akiwa Mfalme juu ya nyumba ya Yakobo milele, na Ufalme wake hautakuwa na mwisho.”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki