-
Ezekieli 21:26, 27Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
26 Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Kiondoe kilemba, na ulivue taji.+ Hili halitabaki kama lilivyo.+ Mwinue aliye chini,+ na umshushe aliye juu.+ 27 Nitaliharibu, nitaliharibu, nitaliharibu. Nalo halitakuwa la mtu yeyote mpaka yule aliye na haki ya kisheria atakapokuja,+ nami nitampa yeye.’+
-
-
Danieli 4:25Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
25 Utafukuzwa mbali kutoka miongoni mwa wanadamu, utaishi na wanyama wa mwituni, nawe utapewa majani ule kama ng’ombe dume; na utalowa kwa umande wa mbinguni,+ na nyakati saba+ zitapita,+ mpaka utakapojua kwamba Aliye Juu Zaidi ni Mtawala katika ufalme wa wanadamu na kwamba yeye humpa ufalme huo yeyote anayetaka kumpa.+
-