6 Kwa maana mtoto amezaliwa kwetu,+
Tumepewa mwana
Na utawala utakaa juu ya bega lake.+
Jina lake litakuwa Mshauri wa Ajabu,+ Mungu Mwenye Nguvu,+ Baba wa Milele, Mkuu wa Amani.
7 Kwa wingi wa utawala wake
Na amani, hakutakuwa na mwisho,+
Kwenye kiti cha ufalme cha Daudi+ na juu ya ufalme wake
Ili kuuimarisha kabisa+ na kuutegemeza
Kupitia haki+ na uadilifu,+
Kuanzia sasa mpaka milele.
Bidii ya Yehova wa majeshi itafanya hayo.