Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Zaburi 45:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  6 Mungu ni kiti chako cha ufalme milele na milele;+

      Fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya unyoofu.*+

  • Isaya 9:6, 7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  6 Kwa maana mtoto amezaliwa kwetu,+

      Tumepewa mwana

      Na utawala* utakaa juu ya bega lake.+

      Jina lake litakuwa Mshauri wa Ajabu,+ Mungu Mwenye Nguvu,+ Baba wa Milele, Mkuu wa Amani.

       7 Kwa wingi wa utawala wake*

      Na amani, hakutakuwa na mwisho,+

      Kwenye kiti cha ufalme cha Daudi+ na juu ya ufalme wake

      Ili kuuimarisha kabisa+ na kuutegemeza

      Kupitia haki+ na uadilifu,+

      Kuanzia sasa mpaka milele.

      Bidii ya Yehova wa majeshi itafanya hayo.

  • Danieli 2:44
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 44 “Katika siku za wafalme hao Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme+ ambao hautaangamizwa kamwe.+ Na ufalme huo hautakabidhiwa watu wengine wowote.+ Utazipondaponda na kuzikomesha falme hizi zote,+ nao pekee utasimama milele,+

  • Luka 1:32, 33
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 32 Huyo atakuwa mkuu+ naye ataitwa Mwana wa Aliye Juu Zaidi,+ na Yehova* Mungu atampa kiti cha ufalme cha Daudi baba yake,+ 33 naye atatawala akiwa Mfalme juu ya nyumba ya Yakobo milele, na Ufalme wake hautakuwa na mwisho.”+

  • Ufunuo 11:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Malaika wa saba akaipiga tarumbeta yake.+ Na sauti kubwa zikasikika mbinguni, zikisema: “Ufalme wa ulimwengu umekuwa Ufalme wa Bwana wetu+ na wa Kristo wake,+ naye atatawala akiwa mfalme milele na milele.”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki