-
2 Wafalme 17:9-11Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
9 Waisraeli walikuwa wakifuatia mambo ambayo hayakuwa sawa machoni pa Yehova Mungu wao. Wakaendelea kujenga mahali pa juu katika majiji yao yote,+ kuanzia mnara wa walinzi mpaka jiji lenye ngome.* 10 Wakaendelea kujisimamishia nguzo takatifu na miti mitakatifu*+ juu ya kila kilima kirefu na chini ya kila mti wenye majani mengi;+ 11 nao walikuwa wakifukiza moshi wa dhabihu mahali pote pa juu kama yalivyofanya mataifa ambayo Yehova alikuwa ameyapeleka uhamishoni kutoka mbele yao.+ Waliendelea kutenda maovu na kumkasirisha Yehova.
-