Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Wafalme 17:19, 20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 Hata watu wa kabila la Yuda hawakushika amri za Yehova Mungu wao;+ walifuata pia desturi zilizofuatwa na Waisraeli.+ 20 Yehova aliwakataa wazao wote wa Israeli, akawaaibisha na kuwatia mikononi mwa waporaji, mpaka alipowatupa mbali kutoka mbele zake.

  • Ezekieli 23:30, 31
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 30 Utatendewa mambo hayo kwa sababu uliyafuata mbio mataifa kama kahaba,+ kwa sababu ulijichafua kwa sanamu zao zinazochukiza.+ 31 Umeifuata njia ileile aliyoifuata dada yako,+ nami nitakiweka kikombe chake mkononi mwako.’+

  • Amosi 2:4, 5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  4 Yehova anasema hivi:

      ‘Kwa sababu ya maasi matatu ya Yuda,+ na hata manne, sitabadili uamuzi wangu,

      Kwa sababu walikataa sheria* ya Yehova,

      Na kwa sababu hawakufuata masharti yake;+

      Lakini uwongo uleule ambao mababu zao walifuata umewapotosha.+

       5 Kwa hiyo nitaishushia moto Yuda,

      Nao utateketeza kabisa minara ya Yerusalemu yenye ngome.’+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki