Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Samweli 12:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Lakini msipotii sauti ya Yehova na mkiasi agizo la Yehova, mkono wa Yehova utawashambulia ninyi na baba zenu.+

  • 1 Mambo ya Nyakati 28:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 “Nawe, Sulemani mwanangu, mjue Mungu wa baba yako na kumtumikia kwa moyo kamili*+ na kwa nafsi* yenye shangwe;* kwa maana Yehova huichunguza kabisa mioyo yote,+ naye hutambua kila mwelekeo wa fikira.+ Ukimtafuta, atakuruhusu umpate,+ lakini ukimwacha, atakukataa milele.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 36:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Kwa hiyo akamleta mfalme wa Wakaldayo awashambulie,+ ambaye aliwaua wanaume wao vijana kwa upanga+ katika nyumba ya mahali pao patakatifu;+ hakumhurumia kijana wa kiume wala bikira, mzee wala aliye dhaifu.+ Mungu alitia kila kitu mikononi mwake.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 36:19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 Aliiteketeza kabisa nyumba ya Mungu wa kweli,+ akaubomoa ukuta wa Yerusalemu,+ akateketeza kwa moto minara yake yote yenye ngome, na kuharibu kila kitu chenye thamani.+

  • Yeremia 17:27
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 27 “‘“Lakini msiponitii kwa kutoshika siku ya Sabato ikiwa siku takatifu na mkibeba mizigo na kuileta kupitia malango ya Yerusalemu katika siku ya Sabato, nitayawasha moto malango yake, nao hakika utaiteketeza minara yenye ngome ya Yerusalemu+ nao hautazimwa.”’”+

  • Yeremia 37:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Na Wakaldayo watarudi tena na kulishambulia jiji hili na kuliteka na kuliteketeza kwa moto.”+

  • Yeremia 52:12-14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Katika mwezi wa tano, siku ya kumi ya mwezi huo, yaani, mwaka wa 19 wa utawala wa Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni, Nebuzaradani mkuu wa walinzi, aliyekuwa mhudumu wa mfalme wa Babiloni, aliingia Yerusalemu.+ 13 Akateketeza kabisa nyumba ya Yehova,+ nyumba ya* mfalme, na nyumba zote za Yerusalemu; aliteketeza pia kila nyumba kubwa. 14 Na jeshi lote la Wakaldayo lililokuwa pamoja na mkuu wa walinzi lilibomoa kuta zilizozunguka Yerusalemu.+

  • Hosea 8:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Waisraeli wamemsahau Muumba wao+ na kujenga mahekalu,+

      Na watu wa Yuda wamezidisha majiji yenye ngome.+

      Lakini nitashusha moto kwenye majiji yao,

      Nao utateketeza minara iliyo katika kila jiji.”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki