7 Lakini Yehova akamwambia Samweli: “Usitazame sura yake wala urefu wake,+ kwa maana nimemkataa. Kwa kuwa Mungu haoni kama mwanadamu anavyoona, kwa maana mwanadamu huona kinachoonekana kwa macho, lakini Yehova huona ndani ya moyo.”+
17 Ee Mungu wangu, najua vizuri kwamba wewe huuchunguza moyo,+ na kwamba unapendezwa na utimilifu.*+ Kwa unyoofu wa moyo wangu, nimetoa kwa hiari vitu hivi vyote, nami nimefurikwa na shangwe kuwaona watu wako walio hapa wakikutolea matoleo ya hiari.
23 Nami nitawaua watoto wake kwa ugonjwa hatari, hivi kwamba makutaniko yote yatajua kwamba mimi ndiye ninayechunguza mawazo ya ndani kabisa* na mioyo, nami nitampa kila mmoja wenu kulingana na matendo yake.+