Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 28:45
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 45 “Laana hizi zote+ hakika zitawajia na kuwafuatia na kuwatangulia mpaka mtakapokuwa mmeangamizwa,+ kwa sababu hamkuisikiliza sauti ya Yehova Mungu wenu kwa kushika amri zake na sheria zake alizowaamuru.+

  • 2 Wafalme 17:6, 7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Katika mwaka wa tisa wa utawala wa Hoshea, mfalme wa Ashuru aliliteka jiji la Samaria.+ Kisha akawapeleka Waisraeli uhamishoni+ kule Ashuru na kuwaweka katika eneo la Hala na Habori kando ya mto Gozani+ na katika majiji ya Wamedi ili waishi humo.+

      7 Hilo lilitendeka kwa sababu Waisraeli walimtendea dhambi Yehova Mungu wao, aliyewatoa nchini Misri kutoka mikononi mwa Farao mfalme wa Misri.+ Waliabudu* miungu mingine,+

  • Ezekieli 23:4, 5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Yule mkubwa aliitwa Ohola,* na dada yake Oholiba.* Wakawa wangu nao wakazaa wana na mabinti. Kuhusu majina yao, Ohola ni Samaria,+ na Oholiba ni Yerusalemu.

      5 “Ohola akaanza kufanya ukahaba+ alipokuwa wangu. Aliwatamani kwa uchu wapenzi wake,+ majirani zake Waashuru.+

  • Hosea 4:1, 2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Lisikieni neno la Yehova, enyi Waisraeli,

      Kwa maana Yehova ana kesi dhidi ya wakaaji wa nchi,+

      Kwa sababu hakuna ukweli wala upendo mshikamanifu wala ujuzi kumhusu Mungu nchini.+

       2 Viapo vya uwongo na udanganyifu+ na mauaji+

      Na wizi na uzinzi+ umeenea sana,

      Na tendo moja la umwagaji wa damu linafuata tendo lingine la umwagaji wa damu.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki