Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Wafalme 23:15, 16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Alibomoa pia madhabahu iliyokuwa Betheli, mahali pa juu ambapo Yeroboamu mwana wa Nebati alijenga na ambapo palisababisha Waisraeli watende dhambi.+ Baada ya kuibomoa madhabahu hiyo na mahali pa juu, aliteketeza mahali hapo pa juu, akapasagasaga pakawa mavumbi, na kuuteketeza mti mtakatifu.*+

      16 Yosia alipogeuka na kuona makaburi yaliyokuwa mlimani, aliagiza mifupa itolewe katika makaburi hayo na kuteketezwa kwenye madhabahu, akaifanya madhabahu hiyo isifae kwa ibada, kulingana na neno la Yehova lililokuwa limesemwa na mtu wa Mungu wa kweli aliyetabiri kwamba mambo hayo yangetukia.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 31:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 31 Mara tu walipomaliza kufanya mambo hayo yote, Waisraeli wote waliokuwepo wakaenda katika majiji ya Yuda, nao wakazivunjavunja nguzo takatifu,+ wakaikatakata miti mitakatifu,*+ na kubomoa mahali pa juu+ na madhabahu+ katika nchi yote ya Yuda na Benjamini, na pia kule Efraimu na Manase,+ mpaka walipoviharibu kabisa vitu hivyo, kisha Waisraeli wote wakarudi katika majiji yao, kila mmoja kwenye miliki yake.

  • 2 Mambo ya Nyakati 34:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 34 Yosia+ alikuwa na umri wa miaka minane alipoanza kutawala, naye alitawala kwa miaka 31 huko Yerusalemu.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 34:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 alibomoa madhabahu na kupondaponda miti mitakatifu* na sanamu za kuchongwa,+ zikabaki ungaunga; naye akavikatakata vinara vyote vya uvumba katika nchi yote ya Israeli,+ kisha akarudi Yerusalemu.

  • Hosea 10:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  2 Moyo wao una unafiki;*

      Sasa watapatikana na hatia.

      Kuna yule atakayebomoa madhabahu zao na kuharibu nguzo zao.

  • Mika 1:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  6 Nitafanya Samaria kuwa rundo la magofu la shambani,

      Mahali pa kupanda mizabibu;

      Nitayatupa* mawe yake chini bondeni,

      Nami nitaichimbua misingi yake.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki