-
2 Wafalme 23:15, 16Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
15 Alibomoa pia madhabahu iliyokuwa Betheli, mahali pa juu ambapo Yeroboamu mwana wa Nebati alijenga na ambapo palisababisha Waisraeli watende dhambi.+ Baada ya kuibomoa madhabahu hiyo na mahali pa juu, aliteketeza mahali hapo pa juu, akapasagasaga pakawa mavumbi, na kuuteketeza mti mtakatifu.*+
16 Yosia alipogeuka na kuona makaburi yaliyokuwa mlimani, aliagiza mifupa itolewe katika makaburi hayo na kuteketezwa kwenye madhabahu, akaifanya madhabahu hiyo isifae kwa ibada, kulingana na neno la Yehova lililokuwa limesemwa na mtu wa Mungu wa kweli aliyetabiri kwamba mambo hayo yangetukia.+
-
-
2 Mambo ya Nyakati 31:1Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
31 Mara tu walipomaliza kufanya mambo hayo yote, Waisraeli wote waliokuwepo wakaenda katika majiji ya Yuda, nao wakazivunjavunja nguzo takatifu,+ wakaikatakata miti mitakatifu,*+ na kubomoa mahali pa juu+ na madhabahu+ katika nchi yote ya Yuda na Benjamini, na pia kule Efraimu na Manase,+ mpaka walipoviharibu kabisa vitu hivyo, kisha Waisraeli wote wakarudi katika majiji yao, kila mmoja kwenye miliki yake.
-
-
Hosea 10:2Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
Kuna yule atakayebomoa madhabahu zao na kuharibu nguzo zao.
-