Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 34:6, 7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Yehova alipita mbele yake akitangaza: “Mimi Yehova, Yehova, ni Mungu mwenye rehema+ na huruma,*+ si mwepesi wa hasira,+ nina upendo mwingi mshikamanifu*+ na kweli,*+ 7 ninawatendea maelfu kwa upendo mshikamanifu,+ ninasamehe makosa na uovu na dhambi,+ lakini sikosi kamwe kuwaadhibu wenye hatia,+ ninawaadhibu wana na wajukuu kufikia kizazi cha tatu na cha nne kwa sababu ya makosa ya baba zao.”+

  • Isaya 1:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 “Sasa, njooni, na tunyooshe mambo kati yetu,” asema Yehova.+

      “Ingawa dhambi zenu ni kama rangi nyekundu,

      Zitafanywa kuwa nyeupe kama theluji;+

      Ingawa ni nyekundu kama kitambaa chekundu,

      Zitakuwa kama sufu.

  • Isaya 44:22
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 Nitayafuta kabisa makosa yako kama kwa wingu+

      Na dhambi zako kama kwa wingu zito.

      Rudi kwangu, kwa maana nitakukomboa.+

  • Yeremia 50:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 “Siku hizo na wakati huo,” asema Yehova,

      “Hatia ya Israeli itatafutwa,

      Lakini hakutakuwa na hatia yoyote,

      Na dhambi za Yuda hazitapatikana,

      Kwa maana nitawasamehe wale nitakaowaacha wabaki.”+

  • Danieli 9:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Rehema na msamaha ni zako Yehova Mungu wetu,+ kwa maana tumekuasi.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki