Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 28:49-51
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 49 “Yehova ataleta dhidi yenu taifa la mbali,+ kutoka mwisho wa dunia; litawarukia kama tai,+ taifa ambalo hamtaelewa lugha yake,+ 50 taifa lenye uso mkali ambalo haliwajali wazee wala kuwahurumia vijana.+ 51 Watu hao watawala watoto wa mifugo yenu na mazao ya ardhi yenu mpaka mtakapokuwa mmeangamizwa. Hawatawaachia nafaka yoyote, divai mpya wala mafuta, ng’ombe mchanga wala mwanakondoo mpaka watakapokuwa wamewaangamiza.+

  • Yeremia 5:15-17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 “Tazameni, ninaleta dhidi yenu taifa kutoka mbali, Enyi watu wa nyumba ya Israeli,”+ asema Yehova.

      “Ni taifa linalodumu.

      Ni taifa la zamani za kale,

      Taifa ambalo lugha yake hamwijui,

      Na hamwezi kuelewa wanachosema.+

      16 Podo lao ni kama kaburi lililo wazi;

      Wote ni mashujaa.

      17 Watakula mavuno yenu na mkate wenu.+

      Watawala wana wenu na mabinti wenu.

      Watayala makundi yenu na mifugo yenu.

      Wataila mizabibu yenu na mitini yenu.

      Watayaangamiza kwa upanga majiji yenu yenye ngome mnayoyatumaini.”

  • Yeremia 6:22, 23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 Yehova anasema hivi:

      “Tazama! Watu wanakuja kutoka nchi ya kaskazini,

      Na taifa kubwa litaamshwa kutoka sehemu za mbali zaidi za dunia.+

      23 Watashika upinde na mkuki.

      Ni wakatili na hawatakuwa na huruma.

      Sauti yao itanguruma kama bahari,

      Nao wanapanda farasi.+

      Wanajipanga kivita dhidi yako kama mwanamume wa vita, Ee binti ya Sayuni.”

  • Ezekieli 23:22, 23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 “Kwa hiyo, ewe Oholiba, Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Ninawachochea wale waliokupenda+ ambao uliwaacha ukiwa umechukizwa, nami nitawaleta ili wakushambulie kutoka kila upande,+ 23 wana wa Babiloni+ na Wakaldayo+ wote, wanaume wa Pekodi+ na Shoa na Koa, pamoja na wana wote wa Ashuru. Wote ni vijana wanaovutia, magavana na watawala wasaidizi, mashujaa waliochaguliwa moja kwa moja,* wote wakiwa wamepanda farasi.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki