-
Isaya 2:2, 3Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
Mlima wa nyumba ya Yehova
Utaimarishwa kabisa juu ya vilele vya milima,+
Nao utainuliwa juu ya vilima,
Na mataifa yote yatamiminika kwenye mlima huo.+
3 Na watu wa mataifa mengi wataenda na kusema:
“Njooni, twendeni juu kwenye mlima wa Yehova,
Kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo.+
Naye atatufundisha njia zake,
Nasi tutatembea katika vijia vyake.”+
-
-
Zekaria 8:22, 23Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
22 Na mataifa mengi na mataifa yenye nguvu yatakuja Yerusalemu kumtafuta Yehova wa majeshi + na kumsihi Yehova awape kibali chake.’*
23 “Yehova wa majeshi anasema hivi: ‘Siku hizo watu kumi kutoka katika lugha zote za mataifa+ watashika, naam, watashika kwa nguvu joho* la Myahudi,* wakisema: “Tunataka kwenda pamoja nanyi,+ kwa maana tumesikia kwamba Mungu yupo pamoja nanyi.”’”+
-