Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Zaburi 22:27
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 27 Miisho yote ya dunia itakumbuka na kumgeukia Yehova.

      Familia zote za mataifa zitainama chini mbele zako.+

  • Isaya 2:2, 3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  2 Katika siku za mwisho,*

      Mlima wa nyumba ya Yehova

      Utaimarishwa kabisa juu ya vilele vya milima,+

      Nao utainuliwa juu ya vilima,

      Na mataifa yote yatamiminika kwenye mlima huo.+

       3 Na watu wa mataifa mengi wataenda na kusema:

      “Njooni, twendeni juu kwenye mlima wa Yehova,

      Kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo.+

      Naye atatufundisha njia zake,

      Nasi tutatembea katika vijia vyake.”+

      Kwa maana sheria itatoka* Sayuni,

      Na neno la Yehova litatoka Yerusalemu.+

  • Isaya 11:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Siku hiyo mzizi wa Yese+ utasimama kama ishara* kwa ajili ya mataifa.+

      Mataifa yatatafuta mwongozo kutoka kwake,*+

      Na mahali pake pa kupumzikia patakuwa na utukufu.

  • Isaya 55:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  5 Tazama! Utaliita taifa ambalo hulijui,

      Na watu wa taifa ambao hawajakujua watakukimbilia

      Kwa ajili ya Yehova Mungu wako,+ Mtakatifu wa Israeli,

      Kwa sababu atakutukuza.+

  • Isaya 60:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  3 Mataifa yataenda kwenye nuru yako+

      Na wafalme+ kwenye fahari yako inayong’aa.*+

  • Hosea 1:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 “Na Waisraeli* watakuwa wengi kama chembe za mchanga wa bahari, ambao hauwezi kupimwa wala kuhesabiwa.+ Na mahali ambapo Mungu aliwaambia, ‘Ninyi si watu wangu,’+ atawaita, ‘Wana wa Mungu aliye hai.’+

  • Mika 4:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  2 Na mataifa mengi yataenda na kusema:

      “Njooni, twendeni juu kwenye mlima wa Yehova

      Na kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo.+

      Naye atatufundisha njia zake,

      Nasi tutatembea katika vijia vyake.”

      Kwa maana sheria itatoka* Sayuni,

      Na neno la Yehova litatoka Yerusalemu.

  • Hagai 2:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 “‘Nami nitayatikisa mataifa yote, na vitu vyenye thamani* vya mataifa yote vitaingia katika nyumba hii;+ nami nitaijaza nyumba hii utukufu,’+ asema Yehova wa majeshi.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki