-
Mathayo 3:1-3Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
3 Siku hizo Yohana+ Mbatizaji alikuja kuhubiri+ katika nyika ya Yudea, 2 akisema: “Tubuni, kwa maana Ufalme wa mbinguni umekaribia.”+ 3 Kwa kweli, huyu ndiye anayezungumziwa kupitia nabii Isaya+ kwa maneno haya: “Kuna mtu anayepaza sauti nyikani: ‘Tayarisheni njia ya Yehova!* Nyoosheni barabara zake.’”+
-
-
Marko 1:2-4Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
2 Kama ilivyoandikwa katika nabii Isaya: “(Tazama! Ninamtuma mjumbe wangu mbele yako,* ili akutayarishie njia.)+ 3 Kuna mtu anayepaza sauti nyikani: ‘Tayarisheni njia ya Yehova!* Nyoosheni barabara zake.’”+ 4 Yohana Mbatizaji alikuwa nyikani, akiwahubiria watu wabatizwe ili kuonyesha kwamba wametubu na hivyo wasamehewe dhambi zao.+
-