-
Marko 4:37-41Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
37 Dhoruba kali ya upepo ikaanza kuvuma, mawimbi yakaipiga mashua, hivi kwamba ikakaribia kuzama.+ 38 Lakini Yesu alikuwa kwenye tezi, akiwa amelalia mto. Basi wakamwamsha na kumwambia: “Mwalimu, je, hujali kwamba tunakaribia kuangamia?” 39 Ndipo akasimama, akaukemea upepo na kuiambia bahari: “Nyamaza! Tulia!”+ Upepo ukakoma, kukawa shwari kabisa. 40 Basi akawauliza: “Kwa nini mnaogopa sana?* Je, bado hamna imani?” 41 Lakini wakaogopa sana, nao wakaulizana: “Kwa kweli, mtu huyu ni nani, hivi kwamba upepo na bahari vinamtii?”+
-
-
Luka 8:23-25Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
23 Walipokuwa wakisafiri akalala usingizi. Dhoruba kali ya upepo ikatokea kwenye ziwa na mashua yao ikaanza kujaa maji ikakaribia kuzama.+ 24 Basi wakaenda kumwamsha na kusema: “Mwalimu, Mwalimu, tuko karibu kuangamia!” Ndipo akasimama, akaukemea upepo na mawimbi ya maji, nayo dhoruba ikatulia, kukawa shwari.+ 25 Kisha akawauliza: “Kwa nini hamna imani?” Lakini wakaogopa na kushangaa, wakaambiana: “Kwa kweli, mtu huyu ni nani? Kwa maana anaamuru upepo na maji, navyo vinamtii.”+
-