Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mathayo 8:24-27
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 Na tazama! dhoruba kubwa ikatokea baharini, hata mawimbi yakaanza kuifunika mashua; lakini Yesu alikuwa amelala usingizi.+ 25 Wakaja na kumwamsha wakisema: “Bwana, tuokoe, tuko karibu kuangamia!” 26 Lakini akawauliza: “Kwa nini mnaogopa sana, ninyi wenye imani ndogo?”+ Kisha akasimama na kuukemea upepo na bahari, kukawa shwari kabisa.+ 27 Basi wanafunzi wakashangaa na kusema: “Huyu ni mtu wa aina gani? Hata upepo na bahari vinamtii.”

  • Luka 8:23-25
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 23 Walipokuwa wakisafiri akalala usingizi. Dhoruba kali ya upepo ikatokea kwenye ziwa na mashua yao ikaanza kujaa maji ikakaribia kuzama.+ 24 Basi wakaenda kumwamsha na kusema: “Mwalimu, Mwalimu, tuko karibu kuangamia!” Ndipo akasimama, akaukemea upepo na mawimbi ya maji, nayo dhoruba ikatulia, kukawa shwari.+ 25 Kisha akawauliza: “Kwa nini hamna imani?” Lakini wakaogopa na kushangaa, wakaambiana: “Kwa kweli, mtu huyu ni nani? Kwa maana anaamuru upepo na maji, navyo vinamtii.”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki