Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mathayo 8:24-27
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 Na tazama! dhoruba kubwa ikatokea baharini, hata mawimbi yakaanza kuifunika mashua; lakini Yesu alikuwa amelala usingizi.+ 25 Wakaja na kumwamsha wakisema: “Bwana, tuokoe, tuko karibu kuangamia!” 26 Lakini akawauliza: “Kwa nini mnaogopa sana, ninyi wenye imani ndogo?”+ Kisha akasimama na kuukemea upepo na bahari, kukawa shwari kabisa.+ 27 Basi wanafunzi wakashangaa na kusema: “Huyu ni mtu wa aina gani? Hata upepo na bahari vinamtii.”

  • Marko 4:37-41
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 37 Dhoruba kali ya upepo ikaanza kuvuma, mawimbi yakaipiga mashua, hivi kwamba ikakaribia kuzama.+ 38 Lakini Yesu alikuwa kwenye tezi, akiwa amelalia mto. Basi wakamwamsha na kumwambia: “Mwalimu, je, hujali kwamba tunakaribia kuangamia?” 39 Ndipo akasimama, akaukemea upepo na kuiambia bahari: “Nyamaza! Tulia!”+ Upepo ukakoma, kukawa shwari kabisa. 40 Basi akawauliza: “Kwa nini mnaogopa sana?* Je, bado hamna imani?” 41 Lakini wakaogopa sana, nao wakaulizana: “Kwa kweli, mtu huyu ni nani, hivi kwamba upepo na bahari vinamtii?”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki