Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 12:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Siku ya kwanza mtakuwa na kusanyiko takatifu, na siku ya saba, mtakuwa na kusanyiko lingine takatifu. Hampaswi kufanya kazi yoyote siku hizo.+ Mtatayarisha tu chakula kitakacholiwa na kila mtu.

  • Kumbukumbu la Torati 23:25
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 25 “Ukiingia katika shamba la nafaka la jirani yako, unaweza kukwanyua kwa mkono wako masuke yaliyokomaa, lakini hupaswi kutumia mundu kukata nafaka ya jirani yako.+

  • Marko 2:23-28
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 23 Alipokuwa akipita kwenye mashamba ya nafaka siku ya Sabato, wanafunzi wake wakaanza kukata masuke ya nafaka huku wakitembea.+ 24 Hivyo, Mafarisayo wakamwambia: “Tazama sasa! Kwa nini wanafanya jambo lisilo halali siku ya Sabato?” 25 Lakini akawaambia: “Je, hamjasoma alilofanya Daudi, wakati alipokuwa na uhitaji na yeye na wanaume waliokuwa pamoja naye walipohisi njaa?+ 26 Jinsi katika simulizi kuhusu mkuu wa makuhani Abiathari,+ Daudi alivyoingia katika nyumba ya Mungu na kula mikate ya toleo,* ambayo si halali kwa mtu yeyote kula isipokuwa makuhani,+ naye akawapa pia watu waliokuwa pamoja naye?” 27 Kisha akawaambia: “Sabato iliwekwa kwa ajili ya mwanadamu,+ bali si mwanadamu kwa ajili ya Sabato. 28 Basi, Mwana wa binadamu pia ndiye Bwana wa Sabato.”+

  • Luka 6:1-5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Siku moja ya Sabato Yesu alipokuwa akipita katika mashamba ya nafaka, wanafunzi wake walikuwa wakivunja na kula masuke ya nafaka, + wakiyapukusa kwa mikono yao.+ 2 Ndipo baadhi ya Mafarisayo wakauliza: “Kwa nini mnafanya jambo lisilo halali siku ya Sabato?”+ 3 Lakini Yesu akawajibu: “Je, hamjasoma alilofanya Daudi wakati yeye na wanaume waliokuwa pamoja naye walipohisi njaa?+ 4 Jinsi alivyoingia katika nyumba ya Mungu akapokea mikate ya toleo,* akala na pia akawapa wanaume waliokuwa pamoja naye, mikate ambayo si halali kwa yeyote kula ila makuhani tu?”+ 5 Kisha akawaambia: “Mwana wa binadamu ndiye Bwana wa Sabato.”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki