-
Marko 2:23-28Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
23 Alipokuwa akipita kwenye mashamba ya nafaka siku ya Sabato, wanafunzi wake wakaanza kukata masuke ya nafaka huku wakitembea.+ 24 Hivyo, Mafarisayo wakamwambia: “Tazama sasa! Kwa nini wanafanya jambo lisilo halali siku ya Sabato?” 25 Lakini akawaambia: “Je, hamjasoma alilofanya Daudi, wakati alipokuwa na uhitaji na yeye na wanaume waliokuwa pamoja naye walipohisi njaa?+ 26 Jinsi katika simulizi kuhusu mkuu wa makuhani Abiathari,+ Daudi alivyoingia katika nyumba ya Mungu na kula mikate ya toleo,* ambayo si halali kwa mtu yeyote kula isipokuwa makuhani,+ naye akawapa pia watu waliokuwa pamoja naye?” 27 Kisha akawaambia: “Sabato iliwekwa kwa ajili ya mwanadamu,+ bali si mwanadamu kwa ajili ya Sabato. 28 Basi, Mwana wa binadamu pia ndiye Bwana wa Sabato.”+
-
-
Luka 6:1-5Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
6 Siku moja ya Sabato Yesu alipokuwa akipita katika mashamba ya nafaka, wanafunzi wake walikuwa wakivunja na kula masuke ya nafaka, + wakiyapukusa kwa mikono yao.+ 2 Ndipo baadhi ya Mafarisayo wakauliza: “Kwa nini mnafanya jambo lisilo halali siku ya Sabato?”+ 3 Lakini Yesu akawajibu: “Je, hamjasoma alilofanya Daudi wakati yeye na wanaume waliokuwa pamoja naye walipohisi njaa?+ 4 Jinsi alivyoingia katika nyumba ya Mungu akapokea mikate ya toleo,* akala na pia akawapa wanaume waliokuwa pamoja naye, mikate ambayo si halali kwa yeyote kula ila makuhani tu?”+ 5 Kisha akawaambia: “Mwana wa binadamu ndiye Bwana wa Sabato.”+
-