-
Mathayo 12:1-8Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
12 Wakati huo, Yesu alipitia katikati ya mashamba ya nafaka siku ya Sabato. Wanafunzi wake wakahisi njaa wakaanza kukata masuke ya nafaka na kula.+ 2 Mafarisayo walipoona hilo, wakamwambia: “Tazama! Wanafunzi wako wanafanya jambo lisilo halali siku ya Sabato.”+ 3 Yesu akawaambia: “Je, hamjasoma alilofanya Daudi wakati yeye na wanaume waliokuwa pamoja naye walipohisi njaa?+ 4 Jinsi alivyoingia katika nyumba ya Mungu, nao wakala mikate ya toleo,*+ kitu ambacho hakikuwa halali kwake au kwa wale waliokuwa pamoja naye kula, ila makuhani tu?+ 5 Au, je, hamjasoma katika Sheria kwamba siku ya Sabato makuhani huvunja Sabato na wanabaki bila hatia?+ 6 Lakini ninawaambia, hapa pana mtu mkuu kuliko hekalu.+ 7 Hata hivyo, kama mngeelewa maana ya maneno haya, ‘Ninataka rehema+ si dhabihu,’+ hamngewalaumu watu wasio na hatia. 8 Kwa maana Mwana wa binadamu ndiye Bwana wa Sabato.”+
-
-
Luka 6:1-5Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
6 Siku moja ya Sabato Yesu alipokuwa akipita katika mashamba ya nafaka, wanafunzi wake walikuwa wakivunja na kula masuke ya nafaka, + wakiyapukusa kwa mikono yao.+ 2 Ndipo baadhi ya Mafarisayo wakauliza: “Kwa nini mnafanya jambo lisilo halali siku ya Sabato?”+ 3 Lakini Yesu akawajibu: “Je, hamjasoma alilofanya Daudi wakati yeye na wanaume waliokuwa pamoja naye walipohisi njaa?+ 4 Jinsi alivyoingia katika nyumba ya Mungu akapokea mikate ya toleo,* akala na pia akawapa wanaume waliokuwa pamoja naye, mikate ambayo si halali kwa yeyote kula ila makuhani tu?”+ 5 Kisha akawaambia: “Mwana wa binadamu ndiye Bwana wa Sabato.”+
-