-
Marko 8:27-29Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
27 Yesu na wanafunzi wake wakaelekea kwenye vijiji vya Kaisaria Filipi, na wakiwa njiani, Yesu akaanza kuwauliza wanafunzi wake: “Watu wanasema mimi ni nani?”+ 28 Wakamjibu: “Yohana Mbatizaji,+ lakini wengine Eliya,+ na bado wengine mmoja wa manabii.” 29 Naye akawauliza: “Hata hivyo, ninyi mnasema mimi ni nani?” Petro akajibu: “Wewe ndiye Kristo.”+
-
-
Luka 9:18-20Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
18 Baadaye, alipokuwa akisali akiwa peke yake, wanafunzi wakaja, naye akawauliza: “Umati unasema mimi ni nani?”+ 19 Wakamjibu: “Yohana Mbatizaji, lakini wengine wanasema Eliya, na bado wengine husema mmoja wa manabii wa kale amefufuliwa.”+ 20 Ndipo akawauliza: “Hata hivyo, ninyi mnasema mimi ni nani?” Petro akajibu: “Kristo wa Mungu.”+
-