13 Alipofika katika eneo la Kaisaria Filipi, Yesu akawauliza wanafunzi wake: “Watu wanasema Mwana wa binadamu ni nani?”+14 Wakajibu: “Baadhi yao husema Yohana Mbatizaji,+ wengine Eliya,+ na bado wengine Yeremia au mmoja wa manabii.” 15 Akawauliza: “Hata hivyo, ninyi mnasema mimi ni nani?”
18 Baadaye, alipokuwa akisali akiwa peke yake, wanafunzi wakaja, naye akawauliza: “Umati unasema mimi ni nani?”+19 Wakamjibu: “Yohana Mbatizaji, lakini wengine wanasema Eliya, na bado wengine husema mmoja wa manabii wa kale amefufuliwa.”+