-
Mathayo 16:13-16Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
13 Alipofika katika eneo la Kaisaria Filipi, Yesu akawauliza wanafunzi wake: “Watu wanasema Mwana wa binadamu ni nani?”+ 14 Wakajibu: “Baadhi yao husema Yohana Mbatizaji,+ wengine Eliya,+ na bado wengine Yeremia au mmoja wa manabii.” 15 Akawauliza: “Hata hivyo, ninyi mnasema mimi ni nani?” 16 Simoni Petro akajibu: “Wewe ndiye Kristo,+ Mwana wa Mungu aliye hai.”+
-
-
Marko 8:27-30Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
27 Yesu na wanafunzi wake wakaelekea kwenye vijiji vya Kaisaria Filipi, na wakiwa njiani, Yesu akaanza kuwauliza wanafunzi wake: “Watu wanasema mimi ni nani?”+ 28 Wakamjibu: “Yohana Mbatizaji,+ lakini wengine Eliya,+ na bado wengine mmoja wa manabii.” 29 Naye akawauliza: “Hata hivyo, ninyi mnasema mimi ni nani?” Petro akajibu: “Wewe ndiye Kristo.”+ 30 Ndipo akawaamuru wasimwambie mtu yeyote kumhusu.+
-