-
Yohana 18:25-27Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
25 Sasa Simoni Petro alikuwa amesimama hapo akiota moto. Ndipo wakamwambia: “Wewe pia ni mmoja wa wanafunzi wake, sivyo?” Akakana na kusema: “Hapana.”+ 26 Mmoja wa watumwa wa kuhani mkuu, aliyekuwa mtu wa ukoo wa yule aliyekatwa sikio+ na Petro, akasema: “Nilikuona katika bustani pamoja naye, sivyo?” 27 Hata hivyo, Petro akakana tena, na papo hapo jogoo akawika.+
-