Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mathayo 8:30-33
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 30 Lakini kule mbali nao kulikuwa na kundi la nguruwe wengi wakila.+ 31 Kwa hiyo wale roho waovu wakaanza kumsihi: “Ukitufukuza, turuhusu tuingie katika lile kundi la nguruwe.”+ 32 Basi akawaambia: “Nendeni!” Ndipo wakatoka na kuingia ndani ya wale nguruwe, na tazama! kundi zima likatimua mbio, likaruka poromoko* likazama baharini na kufa maji. 33 Lakini wachungaji wakakimbia, na walipoingia jijini, wakasimulia mambo yote, kutia ndani habari kuhusu wale watu waliokuwa na roho waovu.

  • Luka 8:32-34
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 32 Sasa kulikuwa na kundi kubwa la nguruwe+ waliokuwa wakila mlimani, basi wakamsihi awaruhusu waingie ndani ya nguruwe hao, naye akawaruhusu.+ 33 Ndipo wale roho waovu wakamtoka mtu huyo na kuingia ndani ya wale nguruwe, kisha lile kundi likatimua mbio, likaruka poromoko,* likazama ndani ya ziwa na kufa maji. 34 Wachungaji walipoona kilichotokea, wakakimbia na kupeleka habari hizo jijini na mashambani.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki