-
Mathayo 8:30-34Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
30 Lakini kule mbali nao kulikuwa na kundi la nguruwe wengi wakila.+ 31 Kwa hiyo wale roho waovu wakaanza kumsihi: “Ukitufukuza, turuhusu tuingie katika lile kundi la nguruwe.”+ 32 Basi akawaambia: “Nendeni!” Ndipo wakatoka na kuingia ndani ya wale nguruwe, na tazama! kundi zima likatimua mbio, likaruka poromoko* likazama baharini na kufa maji. 33 Lakini wachungaji wakakimbia, na walipoingia jijini, wakasimulia mambo yote, kutia ndani habari kuhusu wale watu waliokuwa na roho waovu. 34 Na tazama! watu wote katika jiji hilo wakaenda kukutana na Yesu, na walipomwona, wakamsihi aondoke katika eneo lao.+
-
-
Marko 5:11-17Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
11 Sasa kulikuwa na nguruwe wengi+ wakila hapo mlimani.+ 12 Basi hao roho waovu wakamsihi: “Turuhusu tuingie ndani ya wale nguruwe.” 13 Naye akawaruhusu. Ndipo wale roho waovu wakatoka na kuingia ndani ya wale nguruwe, kisha lile kundi likatimua mbio, likaruka poromoko* na kuzama baharini. Walikuwa karibu 2,000, nao wakafa maji baharini. 14 Lakini wachungaji wa nguruwe hao wakakimbia wakapeleka habari jijini na mashambani, watu wakaja kuona kilichotukia.+ 15 Basi wakamjia Yesu, wakamwona yule mtu aliyekuwa na roho waovu, ambaye mwanzoni alikuwa na kile kikosi, akiwa ameketi, amevaa nguo, na akiwa na akili timamu, nao wakaogopa. 16 Pia, wale walioona tukio hilo wakawasimulia mambo yaliyompata mtu huyo aliyekuwa na roho waovu na kuhusu wale nguruwe. 17 Basi wakaanza kumsihi Yesu aondoke katika eneo lao.+
-