Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mathayo 16:5-12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 Sasa wanafunzi wakavuka kwenda ng’ambo ya bahari lakini wakasahau kuchukua mikate.+ 6 Yesu akawaambia: “Muwe macho na mjihadhari na chachu ya Mafarisayo na Masadukayo.”+ 7 Basi wakaanza kujadiliana, wakisema: “Hatukubeba mikate yoyote.” 8 Akijua hilo, Yesu akawauliza: “Ninyi wenye imani ndogo, kwa nini mnajadiliana kati yenu kuhusu kutokuwa na mikate? 9 Je, bado hamwelewi, au je, hamkumbuki ile mikate mitano kuhusiana na wale watu 5,000, na ni vikapu vingapi mlivyokusanya?+ 10 Au ile mikate saba kuhusiana na wale watu 4,000 na ni vikapu vingapi vikubwa mlivyokusanya?+ 11 Kwa nini hamwelewi kwamba sikuongea nanyi kuhusu mikate? Bali jihadharini na chachu* ya Mafarisayo na Masadukayo.”+ 12 Ndipo wakaelewa kwamba hakuwa akizungumza kuhusu chachu ya mikate, bali kujihadhari na mafundisho ya Mafarisayo na Masadukayo.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki