21 Tangu wakati huo, Yesu akaanza kuwafafanulia wanafunzi wake kwamba ni lazima aende Yerusalemu na kuteswa sana na wazee, wakuu wa makuhani, na waandishi, kisha atauawa, na siku ya tatu afufuliwe.+
22 Walipokuwa wamekusanyika huko Galilaya, Yesu akawaambia: “Mwana wa binadamu atasalitiwa mikononi mwa watu,+23 nao watamuua, na siku ya tatu atafufuliwa.”+ Kwa hiyo wakahuzunika sana.
31 Pia, akaanza kuwafundisha kwamba Mwana wa binadamu lazima apatwe na mateso mengi na kukataliwa na wazee, wakuu wa makuhani, na waandishi, kisha atauawa,+ na baada ya siku tatu atafufuliwa.+
44 “Sikilizeni kwa makini na mkumbuke maneno haya, kwa maana Mwana wa binadamu atasalitiwa mikononi mwa watu.”+45 Lakini hawakuelewa maneno hayo. Kwa kweli, yalifichwa ili wasiyafahamu, nao waliogopa kumuuliza kuhusu maneno hayo.