27Ilipofika asubuhi, wakuu wote wa makuhani na wazee wa watu wakashauriana pamoja kumhusu Yesu ili auawe.+2 Baada ya kumfunga, wakampeleka na kumkabidhi kwa Pilato, gavana.+
66 Kulipokuwa mchana, kikundi cha wazee wa watu, yaani, wakuu wa makuhani na waandishi, wakakusanyika pamoja,+ nao wakampeleka katika jumba lao la Sanhedrini, na kumwambia:
28 Kisha wakamtoa Yesu kwa Kayafa na kumpeleka kwenye makao ya gavana.+ Ilikuwa asubuhi mapema. Lakini wao hawakuingia ndani ya makao ya gavana, ili wasitiwe unajisi+ kwa sababu walitaka kula mlo wa Pasaka.
13 Mungu wa Abrahamu na wa Isaka na wa Yakobo,+ Mungu wa mababu zetu, amemtukuza Mtumishi wake,+ Yesu,+ ambaye ninyi mlimkabidhi+ na kumkana mbele ya Pilato, ingawa alikuwa ameamua kumfungua.