-
Mathayo 27:20-23Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
20 Lakini wakuu wa makuhani na wazee wakaushawishi umati uombe Baraba afunguliwe,+ lakini Yesu auawe.+ 21 Gavana akawauliza: “Mnataka niwafungulie nani kati ya hawa wawili?” Wakasema: “Baraba.” 22 Pilato akawaambia: “Basi, nifanye nini na Yesu anayeitwa Kristo?” Wote wakasema: “Atundikwe mtini!”*+ 23 Akawauliza: “Kwa nini? Amefanya kosa gani?” Wakaendelea kusema kwa sauti kubwa hata zaidi: “Atundikwe mtini!”+
-