-
Mathayo 21:33-41Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
33 “Sikilizeni mfano mwingine: Kulikuwa na mtu aliyemiliki shamba, akapanda shamba la mizabibu+ na kulizungushia ua, akachimba shinikizo la divai* ndani yake, akajenga mnara;+ kisha akalikodisha kwa wakulima, naye akasafiri kwenda ng’ambo.+ 34 Majira ya matunda yalipofika, akawatuma watumwa wake kwa wakulima ili wakachukue matunda yake. 35 Hata hivyo, wakulima hao wakawakamata wale watumwa, mmoja wakampiga, mwingine wakamuua, na mwingine wakampiga mawe.+ 36 Akawatuma tena watumwa wengine, wengi zaidi ya wale wa kwanza, lakini wakawatendea vivyo hivyo.+ 37 Mwishowe akamtuma mwana wake kwao, akisema, ‘Watamheshimu mwanangu.’ 38 Wakulima walipomwona yule mwana wakaambiana, ‘Huyu ndiye mrithi.+ Njooni tumuue ili tuuchukue urithi wake!’ 39 Kwa hiyo wakamkamata, wakamtupa nje ya shamba la mizabibu na kumuua.+ 40 Basi, mwenye shamba la mizabibu atakapokuja, atawatendea nini wakulima hao?” 41 Wakamwambia: “Kwa sababu ni waovu, atawaangamiza kabisa na kulikodisha shamba la mizabibu kwa wakulima wengine, ambao watampa matunda yatakapoiva.”
-
-
Marko 12:1-9Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
12 Akaanza kusema nao kwa mifano: “Mtu fulani alipanda shamba la mizabibu+ akalizungushia ua, akachimba shinikizo la divai, akajenga mnara,+ kisha akalikodisha kwa wakulima, naye akasafiri kwenda ng’ambo.+ 2 Majira yalipofika akamtuma mtumwa kwa wakulima ili achukue kutoka kwao baadhi ya matunda ya shamba la mizabibu. 3 Lakini wakamkamata, wakampiga na kumfukuza mikono mitupu. 4 Akamtuma tena mtumwa mwingine kwao, na huyo wakampiga kichwani na kumwaibisha.+ 5 Akamtuma mwingine, na huyo wakamuua, akawatuma wengine wengi, wakawapiga baadhi yao na kuwaua wengine. 6 Alikuwa na mmoja zaidi, mwana wake mpendwa.+ Mwishowe akamtuma kwao akisema: ‘Watamheshimu mwanangu.’ 7 Lakini wakulima wakaambiana, ‘Huyu ndiye mrithi.+ Njooni tumuue, na urithi utakuwa wetu.’ 8 Kwa hiyo wakamkamata, wakamuua na kumtupa nje ya shamba la mizabibu.+ 9 Mwenye shamba la mizabibu atafanya nini? Atakuja na kuwaua wakulima hao, kisha atawapa watu wengine shamba hilo la mizabibu.+
-