-
Marko 12:1-9Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
12 Akaanza kusema nao kwa mifano: “Mtu fulani alipanda shamba la mizabibu+ akalizungushia ua, akachimba shinikizo la divai, akajenga mnara,+ kisha akalikodisha kwa wakulima, naye akasafiri kwenda ng’ambo.+ 2 Majira yalipofika akamtuma mtumwa kwa wakulima ili achukue kutoka kwao baadhi ya matunda ya shamba la mizabibu. 3 Lakini wakamkamata, wakampiga na kumfukuza mikono mitupu. 4 Akamtuma tena mtumwa mwingine kwao, na huyo wakampiga kichwani na kumwaibisha.+ 5 Akamtuma mwingine, na huyo wakamuua, akawatuma wengine wengi, wakawapiga baadhi yao na kuwaua wengine. 6 Alikuwa na mmoja zaidi, mwana wake mpendwa.+ Mwishowe akamtuma kwao akisema: ‘Watamheshimu mwanangu.’ 7 Lakini wakulima wakaambiana, ‘Huyu ndiye mrithi.+ Njooni tumuue, na urithi utakuwa wetu.’ 8 Kwa hiyo wakamkamata, wakamuua na kumtupa nje ya shamba la mizabibu.+ 9 Mwenye shamba la mizabibu atafanya nini? Atakuja na kuwaua wakulima hao, kisha atawapa watu wengine shamba hilo la mizabibu.+
-
-
Luka 20:9-16Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
9 Yesu akaanza kuwaambia watu mfano huu: “Mtu fulani alipanda shamba la mizabibu+ akalikodisha kwa wakulima, kisha akasafiri kwenda ng’ambo, akakaa huko muda mrefu.+ 10 Majira yalipofika akamtuma mtumwa kwa wakulima ili wampe baadhi ya matunda ya shamba la mizabibu. Hata hivyo, wale wakulima wakampiga na kumfukuza mikono mitupu.+ 11 Lakini akamtuma mtumwa mwingine. Huyo pia wakampiga, wakamwaibisha,* na kumfukuza mikono mitupu. 12 Bado tena akamtuma wa tatu; huyo pia walimjeruhi na kumtupa nje. 13 Ndipo mwenye shamba la mizabibu akasema, ‘Nifanye nini? Nitamtuma mwanangu mpendwa.+ Labda watamheshimu.’ 14 Wakulima walipomwona wakaambiana, ‘Huyu ndiye mrithi. Basi tumuue, ili urithi wake uwe wetu.’ 15 Wakamtupa nje ya shamba la mizabibu na kumuua.+ Kwa hiyo, mwenye shamba la mizabibu atawafanya nini? 16 Atakuja na kuwaua wakulima hao, kisha atawapa watu wengine shamba hilo la mizabibu.”
Waliposikia hivyo wakasema: “Jambo hilo lisitukie kamwe!”
-