Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Wafalme 17:13, 14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Yehova aliwaonya Waisraeli na watu wa Yuda tena na tena kupitia manabii wake wote na kila mwonaji,+ akisema: “Geukeni na kuacha njia zenu ovu!+ Shikeni amri zangu na maagizo yangu kulingana na sheria yote niliyowaamuru mababu zenu na ambayo niliwapa kupitia watumishi wangu manabii.” 14 Lakini hawakusikiliza, nao wakaendelea kuwa wakaidi kama* mababu zao ambao hawakudhihirisha imani katika Yehova Mungu wao.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 36:15, 16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Yehova Mungu wa mababu zao aliendelea kuwaonya kupitia wajumbe wake, aliwaonya tena na tena, kwa sababu aliwahurumia watu wake na makao yake. 16 Lakini waliendelea kuwadhihaki wajumbe wa Mungu wa kweli,+ wakadharau maneno yake+ na kuwakejeli manabii wake,+ mpaka ghadhabu ya Yehova ilipokuja dhidi ya watu wake,+ hivi kwamba hawangeweza kuponywa.

  • Matendo 7:52
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 52 Ni yupi kati ya manabii ambaye mababu zenu hawakumtesa?+ Ndiyo, waliwaua wale waliotangaza mapema kuhusu kuja kwa yule mwadilifu,+ ambaye ninyi mmemsaliti na kumuua,+

  • Waebrania 11:36, 37
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 36 Ndiyo, wengine walipata jaribu lao kwa kudhihakiwa na kupigwa kwa mijeledi, naam, isitoshe, kwa kufungwa minyororo+ na magerezani.+ 37 Walipigwa mawe,+ walijaribiwa, walikatwa vipande viwili* kwa msumeno, walichinjwa kwa upanga,+ walitembea huku na huku wakiwa wamevaa ngozi za kondoo na ngozi za mbuzi,+ wakiwa katika uhitaji, katika dhiki,+ wakiteswa;+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki