Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Zaburi 118:22
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 Jiwe ambalo wajenzi walilikataa

      Limekuwa jiwe kuu la pembeni.*+

  • Isaya 28:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi:

      “Tazama, ninaweka jiwe lililojaribiwa liwe msingi katika Sayuni,+

      Jiwe la pembeni lenye thamani+ la msingi imara.+

      Hakuna yeyote anayeonyesha imani atakayeshikwa na wasiwasi.+

  • Mathayo 21:42
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 42 Yesu akawaambia: “Je, hamkusoma kamwe katika Maandiko kwamba ‘Jiwe ambalo wajenzi walilikataa limekuwa jiwe kuu la pembeni.*+ Hili limetoka kwa Yehova,* na ni lenye kustaajabisha machoni petu’?+

  • Mathayo 21:44
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 44 Pia, mtu atakayeanguka kwenye jiwe hilo atavunjika vipandevipande.+ Na litamponda yeyote litakayemwangukia.”+

  • Marko 12:10, 11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Je, hamkusoma kamwe andiko hili: ‘Jiwe ambalo wajenzi walilikataa, limekuwa jiwe kuu la pembeni.*+ 11 Hili limetoka kwa Yehova,* na ni lenye kustaajabisha machoni petu’?”+

  • Matendo 4:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Hilo ndilo ‘jiwe ambalo ninyi wajenzi mlilitendea kana kwamba halina maana nalo limekuwa jiwe kuu la pembeni.’*+

  • 1 Petro 2:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Kwa hiyo, yeye ni mwenye thamani kwenu, kwa sababu ninyi ni waamini; lakini kwa wale wasioamini, “jiwe ambalo wajenzi walilikataa+ limekuwa jiwe kuu la pembeni”*+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki