Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mathayo 22:23-28
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 23 Siku hiyo, Masadukayo ambao husema hakuna ufufuo,+ wakaja na kumuuliza:+ 24 “Mwalimu, Musa alisema: ‘Mtu yeyote akifa bila kupata watoto, ndugu yake anapaswa kumwoa mke wake ili kumwinulia ndugu yake uzao.’+ 25 Basi kulikuwa na ndugu saba kati yetu. Wa kwanza akaoa kisha akafa, na kwa sababu hakuwa na watoto, akamwachia ndugu yake mke wake. 26 Ikawa vivyo hivyo kwa yule wa pili na wa tatu, na kwa wote saba. 27 Mwishowe, yule mwanamke akafa. 28 Basi, katika ufufuo, atakuwa mke wa nani kati ya wale saba? Kwa maana aliolewa na wote.”

  • Marko 12:18-23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Sasa Masadukayo, ambao husema hakuna ufufuo,+ wakaja na kumuuliza:+ 19 “Mwalimu, Musa alituandikia kwamba mtu akifa na kuacha mke lakini hakuacha mtoto, ndugu yake anapaswa kumchukua mke huyo ili kumwinulia ndugu yake uzao.+ 20 Kulikuwa na ndugu saba. Wa kwanza alioa mwanamke, lakini alipokufa hakuacha uzao wowote. 21 Wa pili akamwoa, lakini akafa bila kuacha uzao, na wa tatu vivyo hivyo. 22 Na wote saba hawakuacha uzao. Mwishowe pia yule mwanamke akafa. 23 Katika ufufuo atakuwa mke wa nani? Kwa maana wote saba walikuwa wamemwoa.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki