14 Ndipo mmoja wa wale 12, aliyeitwa Yuda Iskariote,+ akaenda kwa wakuu wa makuhani+15 na kuwauliza: “Mtanipa nini ili nimsaliti kwenu?”+ Wakakubaliana naye vipande 30 vya fedha.+16 Basi tangu wakati huo akaanza kutafuta nafasi nzuri ya kumsaliti.
10 Yuda Iskariote, mmoja wa wale 12, akaenda kwa wakuu wa makuhani ili amsaliti kwao.+11 Waliposikia hilo, wakafurahi na kuahidi kumpa fedha.+ Basi akaanza kutafuta nafasi ya kumsaliti.
16 “Wanaume, akina ndugu, ilikuwa lazima andiko litimizwe, ambalo roho takatifu ilisema kinabii kupitia Daudi kumhusu Yuda,+ aliyewaongoza wale waliomkamata Yesu.+17 Kwa maana alihesabiwa miongoni mwetu+ naye alipata fungu katika huduma hii.