-
Luka 6:12-16Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
12 Siku moja, Yesu alienda mlimani kusali,+ naye akasali kwa Mungu usiku wote.+ 13 Kulipokucha akawaita wanafunzi wake na kuchagua 12 kati yao, ambao pia aliwaita mitume:+ 14 Simoni, ambaye pia alimwita jina Petro, Andrea ndugu yake, Yakobo, Yohana, Filipo,+ Bartholomayo, 15 Mathayo, Tomasi,+ Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni anayeitwa “mwenye bidii,” 16 Yuda mwana wa Yakobo, na Yuda Iskariote, aliyegeuka kuwa msaliti.
-