-
Kumbukumbu la Torati 12:5, 6Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
5 Badala yake, mtafuteni Yehova Mungu wenu mahali popote atakapochagua kuweka jina lake na mahali atakapokaa miongoni mwa makabila yote, mwende mahali hapo.+ 6 Hapo ndipo mnapopaswa kupeleka dhabihu zenu za kuteketezwa,+ matoleo yenu, sehemu zenu za kumi,+ mchango kutoka mkononi mwenu,+ dhabihu zenu za nadhiri, matoleo yenu ya hiari,+ na wazaliwa wa kwanza wa ng’ombe na kondoo wenu.+
-
-
Zaburi 122:utangulizi-9Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
Wimbo wa Safari za Kupanda. Wa Daudi.
122 Nilishangilia waliponiambia:
“Na twende katika nyumba ya Yehova.”+
4 Makabila yamepanda kwenda humo,
Makabila ya Yah,*
Kulingana na kikumbusho walichopewa Waisraeli,
Ili walishukuru jina la Yehova.+
6 Ombeni ili Yerusalemu liwe na amani.+
Wale wanaokupenda, Ee jiji, watakuwa salama.
8 Kwa ajili ya ndugu zangu na rafiki zangu nitasema:
“Amani na iwe ndani yako.”
-