Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 12:5, 6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 Badala yake, mtafuteni Yehova Mungu wenu mahali popote atakapochagua kuweka jina lake na mahali atakapokaa miongoni mwa makabila yote, mwende mahali hapo.+ 6 Hapo ndipo mnapopaswa kupeleka dhabihu zenu za kuteketezwa,+ matoleo yenu, sehemu zenu za kumi,+ mchango kutoka mkononi mwenu,+ dhabihu zenu za nadhiri, matoleo yenu ya hiari,+ na wazaliwa wa kwanza wa ng’ombe na kondoo wenu.+

  • 1 Wafalme 9:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Yehova akamwambia: “Nimesikia sala yako na ombi lako la kutaka kibali ulilotoa mbele zangu. Nimeitakasa nyumba hii ambayo umejenga kwa kuliweka jina langu humu milele,+ na macho yangu na moyo wangu utakuwa humu sikuzote.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 7:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Kisha Yehova akamtokea Sulemani+ usiku na kumwambia: “Nimesikia sala yako, nami nimechagua mahali hapa kwa ajili yangu ili pawe nyumba ya dhabihu.+

  • Zaburi 122:utangulizi-9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • Wimbo wa Safari za Kupanda. Wa Daudi.

      122 Nilishangilia waliponiambia:

      “Na twende katika nyumba ya Yehova.”+

       2 Na sasa miguu yetu imesimama

      Ndani ya malango yako, Ee Yerusalemu.+

       3 Yerusalemu limejengwa kama jiji

      Ambalo limeunganishwa pamoja kama kitu kimoja.+

       4 Makabila yamepanda kwenda humo,

      Makabila ya Yah,*

      Kulingana na kikumbusho walichopewa Waisraeli,

      Ili walishukuru jina la Yehova.+

       5 Kwa maana viti vya ufalme vya hukumu viliwekwa huko,+

      Viti vya ufalme vya nyumba ya Daudi.+

       6 Ombeni ili Yerusalemu liwe na amani.+

      Wale wanaokupenda, Ee jiji, watakuwa salama.

       7 Amani na idumu ndani ya maboma yako,*

      Usalama ndani ya minara yako yenye ngome.

       8 Kwa ajili ya ndugu zangu na rafiki zangu nitasema:

      “Amani na iwe ndani yako.”

       9 Kwa ajili ya nyumba ya Yehova Mungu wetu,+

      Nitakutakia mema.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki