Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Hesabu 21:8, 9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Kisha Yehova akamwambia Musa: “Tengeneza mfano wa nyoka mwenye sumu na uuweke juu ya nguzo. Mtu yeyote akiumwa na nyoka, ni lazima autazame mfano huo ili aendelee kuishi.” 9 Mara moja Musa akatengeneza nyoka wa shaba+ na kumweka juu ya nguzo,+ na mtu yeyote aliyeumwa na nyoka na kumtazama nyoka huyo wa shaba, aliendelea kuishi.+

  • Danieli 7:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 “Nikaendelea kuangalia katika maono ya usiku, na tazama! mtu fulani kama mwana wa binadamu+ alikuwa akija na mawingu ya mbinguni; naye akaja mbele za Mzee wa Siku,+ nao wakamleta karibu Naye.

  • Mathayo 26:64
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 64 Yesu akamjibu: “Wewe mwenyewe umesema. Lakini ninawaambia: Tangu sasa mtamwona Mwana wa binadamu+ akiwa ameketi kwenye mkono wa kuume wa nguvu,+ akija juu ya mawingu ya mbinguni.”+

  • Yohana 3:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Kama vile Musa alivyoinua nyoka nyikani,+ ndivyo Mwana wa binadamu atakavyoinuliwa,+

  • Yohana 12:32, 33
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 32 Na bado mimi, nikiinuliwa kutoka duniani,+ nitawavuta watu wa namna zote kwangu.” 33 Kwa kweli alisema hivyo ili kuonyesha ni kifo cha aina gani alikuwa karibu kufa.+

  • Wagalatia 3:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Kristo alitununua,+ akatuweka huru+ kutoka katika laana ya Sheria akawa laana badala yetu, kwa sababu imeandikwa: “Amelaaniwa kila mtu aliyetundikwa kwenye mti.”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki