Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mathayo 5:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Furahini na kushangilia sana,+ kwa kuwa thawabu+ yenu ni kubwa mbinguni, kwa maana hivyo ndivyo walivyowatesa manabii waliokuwapo kabla yenu.+

  • Matendo 16:25
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 25 Lakini karibu katikati ya usiku, Paulo na Sila walikuwa wakisali na kumsifu Mungu kwa wimbo,+ nao wafungwa walikuwa wakiwasikiliza.

  • Waroma 5:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Si hilo tu, bali na tushangilie* tukiwa katika dhiki,+ kwa kuwa tunajua kwamba dhiki hutokeza uvumilivu;+

  • 2 Wakorintho 12:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Basi ninapendezwa na udhaifu, na matusi, na nyakati za uhitaji, na mateso na shida, kwa ajili ya Kristo. Kwa maana ninapokuwa dhaifu, ndipo ninapokuwa na nguvu.+

  • Wafilipi 1:29
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 29 Kwa maana mlipewa pendeleo kwa ajili ya Kristo, si muwe tu na imani katika yeye, bali pia mteseke kwa ajili yake.+

  • Waebrania 10:34
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 34 Kwa maana mliwasikitikia wale waliokuwa gerezani na pia kwa shangwe mkakubali kuporwa mali zenu,+ mkijua kwamba ninyi wenyewe mna urithi* bora na wenye kudumu.+

  • 1 Petro 4:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Badala yake, endeleeni kushangilia+ kwa kadiri ambayo ninyi ni washiriki katika mateso ya Kristo,+ ili mshangilie na kuwa na shangwe sana pia wakati wa ufunuo wa utukufu wake.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki