7 Alikandamizwa+ na alikubali kuteswa,+
Lakini hakuthubutu kufungua kinywa chake.
Aliletwa kama kondoo machinjioni,+
Kama kondoo jike aliye kimya mbele ya wanaomkata manyoya,
Na hakuthubutu kufungua kinywa chake.+
8 Kwa sababu ya kizuizi na hukumu alichukuliwa;
Na ni nani atakayejishughulisha na habari za kizazi chake?
Kwa maana aliondolewa katika nchi ya walio hai;+
Alipata pigo kwa sababu ya makosa ya watu wangu.+