-
Mwanzo 14:17-20Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
17 Abramu aliporudi baada ya kumshinda Kedorlaoma na wafalme waliokuwa pamoja naye, mfalme wa Sodoma alienda kukutana na Abramu kwenye Bonde la* Shave, yaani, Bonde la Mfalme.+ 18 Na Melkizedeki+ mfalme wa Salemu+ akaleta mkate na divai; alikuwa kuhani wa Mungu Aliye Juu Zaidi.+
19 Kisha akambariki Abramu na kumwambia:
“Abramu na abarikiwe na Mungu Aliye Juu Zaidi,
Muumba wa mbingu na dunia;
20 Na asifiwe Mungu Aliye Juu Zaidi,
Ambaye amewatia mikononi mwako wale wanaokukandamiza!”
Na Abramu akampa sehemu ya kumi ya vitu vyote.+
-