Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 15:7, 8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 “Ikiwa mmoja wa ndugu zenu atakuwa maskini miongoni mwenu katika mojawapo ya majiji yaliyo katika nchi ambayo Yehova Mungu wenu anawapa, msiifanye mioyo yenu iwe migumu au kumfumbia mkono ndugu yenu maskini.+ 8 Kwa maana mnapaswa kumfumbulia mkono wenu kwa ukarimu+ na kufanya yote mwezayo kumkopesha* chochote anachohitaji au alichopungukiwa.

  • Mathayo 25:35, 36
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 35 Kwa maana nilikuwa na njaa mkanipa chakula; nilikuwa na kiu mkanipa kinywaji. Nilikuwa mgeni mkanikaribisha vizuri;+ 36 nilikuwa uchi,* mkanivika nguo.+ Nilikuwa mgonjwa mkanitunza. Nilikuwa gerezani mkanitembelea.’+

  • Luka 3:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Akawajibu: “Mtu aliye na mavazi mawili* ampe vazi moja yule ambaye hana, na aliye na chakula afanye vivyo hivyo.”+

  • Waroma 12:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Shirikini pamoja na watakatifu kulingana na mahitaji yao.+ Iweni wakaribishaji wageni.*+

  • 1 Timotheo 5:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Lakini ikiwa mjane yeyote ana watoto au wajukuu, wanapaswa kwanza kujifunza ujitoaji-kimungu* katika nyumba zao wenyewe+ na kuwalipa wazazi wao na wazazi wa wazazi wao kinachowastahili,+ kwa maana hilo linakubalika machoni pa Mungu.+

  • Yakobo 1:27
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 27 Namna ya ibada* iliyo safi na isiyo na unajisi kwa maoni ya Mungu wetu na Baba ni hii: kuwatunza mayatima+ na wajane+ katika dhiki yao,+ na kuendelea kujitunza bila doa kutokana na ulimwengu.+

  • 1 Yohana 3:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Lakini yeyote aliye na mali za ulimwengu huu akimwona ndugu yake akiwa na uhitaji naye akatae kumhurumia, anawezaje kuwa na upendo wa Mungu ndani yake?+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki